Naibu
Katibu Mkuu wa CHADEMA Mh. Zitto Kabwe (Mb) amesema ni jambo la ajabu
serikali kufungia magazeti eti kwasababu limechapisha mishahara ya
watumishi wa Serikali. Zitto amesema Kikwete alisaini mkataba wa uwazi
wa serikali na Rais Obama miezi michache iliyopita, "sasa kunauwazi gani
zaidi ya wananchi kujua mshahara wa Rais wao na Mawaziri" alihoji
Zitto. Sasa niwaambie Wananchi wa Mpanda Waziri Mkuu analipwa takribani
Milioni 26 na hakatwi kodi, halipi kodi ya nyumba, hanunui nguo yaani ni
ajabu. Akifafanua kuhusu mshahara wa Waziri Mkuu Zitto alisema Waziri
Mkuu kama Mbunge analipwa Milioni 11.2, Kama Waziri anaongezewa kama
Milioni 9.8 na kama Waziri Mkuu anaongezewa tena kama milioni 5 alisema
Zitto. Zitto amesema uchochezi unaosemwa na serikali ni tofauti kubwa ya
Mishahara na Kodi kwa Watumishi wa Serikali moja wenye majukumu ambayo
karibia yanafanana na kiwango cha elimu kinayofanana.
Chanzo:Jamiiforum
No comments:
Post a Comment