Tuesday, October 8, 2013

Magufuli,Ubabe katika shughuli za Serikali umepitwa na wakati!

Mh.Magufuli anatakiwa kujua kwamba Watanzania wa sasa sio wale wa zamani ambao mtu angeweza kuwaburuza atakavyo.Sasa hivi Serikali inaendeshwa kwa misingi ya Utawala Bora.Inashangaza kuona Mh. huyu akitoa majigambo na kumdharau Waziri aliyekuwa ametoa waraka kuruhusu magari yatumiayo barabara zetu kupewa msamaha wa uzito unaofikia asilimia tano ya uzito uliowekwa kisheria.Jambo la kujiuliza ni je,Mh Magufuli kauona lini Waraka huo?Mbona upo tangu mwaka 2006 na yeye amekuwa Waziri wa Wizara hiyo tangu lini?Unafiki wa namna hii ni hatari kwa maendeleo ya nchi hasa pale Serikali inapokuwa na viongozi wa aina ya Mh. Magufuli.Kama kulikuwa na nia nzuri ya kuchukua hatua ya kuufuta huo Waraka Mh. Magufuli alishindwa nini kutoa muda kwa wasafirishaji ili wajue kuwa kuanzia tarehe fulani unafuu uliokuwepo utaondolewa.Viongozi wapenda sifa na wenye majigambo wanawaumiza wananchi kwa maamuzi yao ya kipuuzi na yasiyozingatia busara.Kwamba msafirishaji ambaye gari lake tayari liko njiani atarekebisha vipi mzigo alioubeba kabla ya kufika mizani?Hapo kuna utawala bora?Sasa hivi tayari wananchi wameanza kupata adha ya usafiri kutokana na ubabe wa kiongozi asiye na msimamizi!Mtu huyu anasemekana kuwa anautaka uraisi akiupata nchi hii si itaangamia?

chanzo:Jamiiforum

No comments:

Post a Comment